Menu ›
Burudani
Mon, 8 Apr 2024
Chanzo: Rick
Huwezi kuikamilisha historia ya waigizaji Bongo bila kutaja jina la mrembo Mainda, huyu alikuwa alama ya filamu nchini lakini ghafla alipotea kwa miaka mingi sasa!
Mainda ameonekana kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao iliyofanyika katika ukumbi wa Karemjee jijini Dar ambapo kama kawaida, waandishi wakampa kipaza sauti.
"Nilipotea kwa mipango yangu tu binafsi na si kwamba ndoa au familia. Sijaolewa na sina watoto," alisema Mainda.
Alipoulizwa kuhusu umri kusogea na kwamba ana mpango gani wa kuolewa, Mainda alisema wakati sahihi bado haujafika.
Chanzo: Rick