Mshindi wa Tuzo ya Grammy Africa tyla ametia neno watu kumfananisha kimuziki na kimuonekano na staa mkubwa wa muziki na bilionea Rihanna
Mwanamuziki huyo kutoka South Africa Tyla anasema inapendeza kufananishwa na Rihanna kwa sababu watu watazidi kumjua yeye na muziki wake.
“Inapendeza kwa sababu Rihanna ni Rihanna. Ni pongezi lakini wakati huo huo nina usanii wangu mwenyewe. Mimi ni Tyla na najua watu wanavyozidi kunifahamu na muziki wangu wataniona kama Tyla tu. Kwa hivyo niko sawa nayo sasa” amesema Tyla
Tyla amefunguka hilo kupitia jarida la #Cosmopolitan ambalo linadili ni chapa (Brand) kubwa zaidi ya vyombo vya habari vya wanawake vijana ulimwenguni.