Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tyla aahirisha ziara ya dunia kutokana na jeraha

Tyla Aahirisha Ziara Ya Dunia Kutokana Na Jeraha Tyla aahirisha ziara ya dunia kutokana na jeraha

Fri, 8 Mar 2024 Chanzo: Bbc

Nyota wa muziki wa Afrika Kusini, Tyla ameghairi ziara yake ya kwanza ya dunia iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu wiki mbili kabla ya kuanza, kwa sababu ya jeraha.

"Kwa mwaka uliopita nimekuwa nikiugua kimyakimya kutokana na jeraha ambalo limezidi," aliandika kwenye Instagram siku ya Alhamisi, bila kufichua chanzo cha jeraha hilo.

"Nimewaona madaktari na wataalamu lakini maumivu yamezidi kuwa makali," aliongeza.

Tyla, ambaye mwezi uliopita alishinda Grammy kwa wimbo wake maarufu wa Water, alipangiwa kuanza ziara yake tarehe 21 Machi katika mji mkuu wa Norway, Oslo.

Lakini alisema katika chapisho lake kwamba "kuendelea na tamasha au tarehe zozote za ziara kunaweza kuhatarisha afya na usalama wangu ".

Jeraha hilo pia limemlazimu kughairi kuonekana kwake Aprili katika tamasha la muziki la Coachella, ripoti ya vyombo vya habari vya Marekani imeeleza.

Aliongeza kuwa wale walionunua tiketi za tamasha huko Amerika Kaskazini watarejeshewa pesa, huku tarehe zake za ziara nchini Uingereza na Ulaya zikipangwa upya.

Chanzo: Bbc