Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tulishtuka sana baada ya kugundua ni watoto mapacha - Davido

Davido Mapacha Ms Tulishtuka sana baada ya kugundua ni watoto mapacha - Davido

Mon, 16 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwimbaji maarufu, David Adeleke, AKA Davido, amesema kuwa yeye na mkewe, Chioma walikuwa wakitetemeka kwa furaha walipogundua kuwa walikuwa wanatarajia watoto mapacha.

Kumbuka kwamba wanandoa hao Mashuhuri walionekana na mapacha wao wachanga kwa mara ya kwanza kwenye video iliyotolewa Ijumaa.

Akizungumza katika hafla ya United Masters Select Con Jumapili, mwimbaji huyo wa ‘Timeless’ alisema Mungu alimbariki na mapacha mwezi huo huo mwanawe, Ifeanyi alipofariki.

Davido na mkewe walipoteza mtoto wao baada ya tukio la swimmingpool nyumbani kwao mnamo Oktoba 2022.

“Mimi na mke wangu tulipogundua, tulikuwa tunatetemeka, na ilikuwa mwezi huo huo mwanangu alifariki. Mwanangu alifariki mwaka jana Oktoba, na mke wangu alijifungua mwaka huu Oktoba.

“Nilikuwa katika hatua ya kukata tamaa. Mvulana na msichana mrembo walirudi wakiwa wawili. Niliweka imani licha ya kuwa ngumu sana,” alisema

Chanzo: www.tanzaniaweb.live