Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tulia ataja ngoma yake kwenye #FOA

Diamond Tuliaa Tulia ataja ngoma yake kwenye #FOA

Mon, 14 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Dr Tulia Ackosn Mwansasu; ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye naye ameonesha kuguswa na albam fupi (EP) ya Diamond Platnumz ya First Of All (FOA) aliyoiachia mwishoni mwa wiki iliyopita.

Tulia anasema kuwa, ngoma anayoikubali ni Nawaza ambayo ni ngoma namba 8 kati ya 10 zinazopatikana ndani ya EP hiyo.

Tulia anasema; “Kwenye FOA na mimi nina wimbo wangu ambao ni Nawaza. Ni wimbo unaotafakarisha juu ya mambo mbalimbali ambayo anajiuliza Diamond kama yakitokea au asipokuwepo itakuwaje?”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live