Mwanamuziki Tiwa Savage atangaza kutokea kwenye filamu kwa mara ya kwanza kupitia Filamu yake aliyoipa jina la Water&Garri ambayo jina hilo limetokana na EP yake Water&Garry aliyoiachia mwaka 2021.
Tiwa ameshirikiana na Director Meji Arabi huku maudhui makubwa ya Filamu hiyo itakuwa inamuelezea binti ayeamua kurudi nyumbani kwao Nigeria baada ya kujichimbia Marekani kwa takribani miaka 10 akijihusisha na masuala ya mitindo.
Anaporudi nyumbani anakuta hali imebadilika machafuko, amani hakuna kama alivyoacha wakati anaondoka hivyo anajaribu kuweka mambo sawa.
Mpaka sasa haijafahamika ni lini Filamu hiyo itaingizwa sokoni.