Menu ›
Burudani
Wed, 16 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Msanii wa Bongo Movie nchini Tanzania, Chris Lubango amefariki dunia wiki iliyopita baada ya kupata ajali ya gari nchini Marekani.
Lubango aliyekuwa anaishi nchini humo na kufanya kazi za udereva nchini humo amepata ajali hiyo akitokea Texas kwenda Chicago na kupata ajali katika Jiji la Oklahoma.
Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga, Haji Manara ambaye yuko nchini humo amethibitisha taarifa za kifo hicho na kusema familia ya Lubango na Watanzania wanaoishi nchini humo wameanza taratibu za kuusafirisha mwili huo kurudi Tanzania kwa ajili ya shughuli za maziko.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live