Menu ›
Burudani
Wed, 1 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii mkongwe na miongoni mwa washairi wakubwa nchini na Afrika Mashariki, Amir Sudi Andanenga amefariki dunia usiku wa Mei Mosi, 2024.
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Chama cha Usanifu wa Kiswahili na Ushairi nchini (UKUTA), marehemu Andanenga amekutwa na umauti akipatiwa matibabu katika hospitali ya Dkt. Mvungi, Kinondoni, Dar es Salaam.
Maziko ya Andanenga aliyefahamika zaidi kwa jina la sanaa ya ushairi la ‘Sauti ya Kiza’ yanatarajiwa kufanyika leo tarehe mosi, Mei 2024 wilayani Kinondoni Dar es Salaam.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live