Menu ›
Burudani
Sun, 25 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii mkongwe wa Bongo Fleva, Afande Sele 'Mkali wa Rhymes' amefiwa na Mama yake mzazi, Bi. Anna Msaki, ambaye amefariki dunia jana, Jumamosi, Septemba24, 2022.
Kupitia Instagram Sele amethibitisha; “Jana kwenye saa moja jioni nilipokea Taarifa za kifo Cha Mama yangu mzazi Anna Msaki, kutokana na jambo lililotuleta Mtwara” amesema.
“Taarifa hizi zikabaki Kwa wachache ndani ya Tim yetu, tulisubiri tumalize pambano ndipo tuliweke wazi. Rest in Peace Mama,” amesema Afande Sele.
Msiba wa Bi. Msaki upo nyumbani kwake Sanya Juu, wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live