Muziki unalipa na hilo halina ubishi, kwani msanii Tanasha Donna yeye amesema mpaka atakapofikisha miaka 30 yaani miaka 3 ijayo atakuwa amepata Sh2.3 bilioni kutokana na shughuli anazozifanya pamoja na muziki.
Tanasha Donna mwenye umri wa miaka 27 sasa, ameeleza hayo kwenye mahojiano yake nchini kenya.
Pia, amebainisha zipo shughuli zingine anazowekeza ambazo zinaweza kumuingizia Dola 1 milioni kabla ya kufikisha umri huo kwani amewekeza kwenye biashara japo hataki kuonyesha vitu anavyovifanya kwa umma.
Kadhalika na hilo, pia ameweka wazi mwezi ujao anaachia wimbo wake mpya ambao amesema ame-rap kwenye kazi hiyo.