Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tamasha la Sauti za Busara laanza Zanzibar

Tamasha La Sauti Za Busara Laanza Zanzibar Tamasha la Sauti za Busara laanza Zanzibar

Fri, 10 Feb 2023 Chanzo: Bbc

Tamasha la Sauti za Busara limeanza rasmi hii leo katika mji mkongwe wa kisiwa cha karafuu.

Wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wamejawa na shauku ya kutaka kuona tamasha la mwaka huu litakuwa na mvuto kiasi gani, huku wasanii kutoka zaidi ya nchi 12 wamejipanga kutumbuiza mashabiki wenye hamu ya kupata burudani.

Shamra shamza hizi zitarindima kisiwani hapa kwa muda wa siku tatu mfululizo.

Leo hii kinachoanza ni wasanii kuwa jukwaani na kuonyesha umahiri wao, huku kilele cha shughuli hiyo kitakuwa siku ya Jumapili ambapo kiwatakutanisha wasanii, wafadhili, na wadau wengine kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.

Tangu kumalizika kwa janga la korona, hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa mashabiki wa tamasha la Sauti za Busara kujiachia bila hofu ya maambukizi.

Yusuf Mahmoud ambae ndio mwanzilishi wa tamasha hilo, anasema miaka 20 ya kuwepo kwa tamasha hilo, licha ya kuwa na mchango mkubwa katika mzunguko wa fedha kwa wakazi, lakini changamoto vile vile vimekuwa nyingi kiasi cha kuhatarisha kuendelea kuwepo kwa tamasha.

“Kutokana na uhaba wa fedha, mwaka huu kuna baadhi ya vitu tumeshindwa kuviweka katika tamasha, jukwaa la nje, mafunzo kwa wasanii lakini pia matembezi ya mwanzo kabla ya tamasha,” ameiambia BBC.

Kwa mujibu wa Yusuf, mwaka 2020 fedha zilizotumika kufanya tamasha hilo ilikuwa ni dola laki nne, lakini fedha zilizoingia katika mzunguko ni dola milioni 18.3.

Na ni sababu hii ndio inayowafanya wafanyabiashara wadogo wadogo na hata wakubwa kufurahia uwepo wa tamasha.

Hata, kila jema halikosi kasoro, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wakazi wa Unguja kwamba tamasha la Sauti za Busara kwa kiasi fulani linachangia mmomonyoko wa maadili hasa ikizingatiwa, asilimia kubwa ya jamii ya wazanzibari ni waislamu. Hata hivyo, Yusuf anasema, wamekuwa wakizingitia maadili ya wakazi ili kuepusha mikwaruzano.

Chanzo: Bbc