Mtangazaji mkongwe wa Radio hapa Tanzania na mdau mkubwa wa Muziki wa Bongo Fleva, Taji Liundi maarufu kama Master T tajiliundi amesema Mwimbaji Diamond Platnumz diamondplatnumz sio namba 1 kwa sasa kwenye Muziki wa Tanzania.
Kwenye mahojiano na kipindi cha The Classic na Mtangazaji @jabirsalehtherealest wa E-FM, Taji ametoa sababu zake kwamba, Diamond Platnumz anaelekea kwenye kuganda “Stuck” kwa sababu hana kitu kipya kwenye uimbaji wake.
Taji alienda mbali zaidi na kusema [Diamond] leo ana-struggle na hajui amuimbie nani, hivyo pia anatumia mbinu ya kuwaweka karibu wasanii wa sasa kwa sababu ya kuendelea kubaki ‘relevant’ lakini anapaswa kujiangalia sana kwa sababu kwenye TOP 20 ya wasanii wa leo, hayupo namba 1.