Rapa T.I anaamini Rapa Young Thug atashinda kesi inayomkabili na atarudi nyumbani kama kawaida, mkali T.I amefunguka kupitia mahojiano na kipindi cha radio cha “The Breakfast Club” siku ya Jumanne Mei 28, 2024.
T.I amesema ya kuwa, Rapa Young Thug atarudi nyumbani na kuendelea na maisha yake kwa sababu mpaka sasa waendesha mashtaka hawajapata ushahidi juu ya kesi inayomkabili “Sidhani kama mashahidi ambao wamewaita hadi sasa wamethibitisha kile walichosema” Alisema Rapa T.I
Imetimia miaka miwili sasa tangu Rapa Young Thug awe chini ya ulinzi na kufunguliwa kesi dhidi ya umiliki makundi yanayojihusisha na shughuli za uhalifu, Thug na wenzake walikamatwa na polisi Mei 2022, mpaka sasa kesi inayomkabili inaendelea kusikilizwa mahakamani.
Young Thug ni mwanzilishi na mmiliki wa lebo ya muziki inayojulikana kama “YOUNG STONER LIFE RECORDS” YSL inayomiliki wasanii kama Gunna, NBA Young Boy, Lil Duke Na Wengine.