Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Steve Nyerere ahoji Ray, JB, Aunt Ezekiel, Shamsa Ford, Johari, Uwoya, Batuli kutopatiwa Tuzo

5655 Stve N TZW

Tue, 3 Apr 2018 Chanzo: bongo5.com

Baada ya utoaji wa Tuzo za filamu za Sinema Zetu International Film Festival Awards (SZIFF), msanii wa filamu Bongo, Steven Nyerere amesema atazungumza baada ya kuona baadhi ya wasanii ambao anaona walistahili kupata lakini haikuwa hivyo.



Muigizaji huyo amehoji kwanini waigizaji wakubwa kama Ray Kigosi, JB, Aunt Ezekiel, Shamsa Ford, Johari na wengineo kutokuwepo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

“Nitaongea nilichokiona kwenye tuzo, kwanini Ray, JB, Rich, Roams, Aunt Ezekiel, Shamsa Ford, Duma, Weru, Hemedi, Tausi Mndengela, Mainda, Johari, Uwoya, Marian Ismail, Batuli na wengine wanaofanya vizuri wapo wapi ?,” amehoji.

“Na mbona sijawaona na kuna vijana wasanii chipukizi wanafanya vizuri, nini tatizo,” ameongeza.

Soma Pia; Gabo Zigamba, Wema Sepetu wazoa tuzo za SZIFF na kuacha historia 

Katika Tuzo za filamu za Sinema Zetu International Film Festival Award (SZIFF) zilizotolewa April Mosi mwaka huu, miongoni mwa waigizaji waliofanya vizuri ni pamoja na Gabo Zigamba aliyejinyakulia tuzo tano wakati Wema Sepetu alishinda tuzo mbili.

Chanzo: bongo5.com