Menu ›
Burudani
Fri, 16 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Steve Nyerere; ni mchekeshaji wa Bongo Movies na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao ambaye siku chache baada ya kusema kuwa tozo ni muhimu kwa kila Mtanzania ili maendeleo yapatikane, sasa amekuja na nyingine kuhusu ishu hiyo.
Steve anasema kuwa, anajua Serikali imekaa kuangalia namna ya kutoza tozo hizo, lakini kwa upande wake anaomba sana tozo hizo zipungue hasa zile ndogondogo, halafu zibaki zile kubwakubwa za mabenki.
Anasema kuwa, hatua hiyo itawapa nafuu Watanzania ambao wamekuwa wakizilalamikia tozo hizo na anaamini Serikali ni sikivu hivyo itakuwa imesikia kilio chao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live