Menu ›
Burudani
Fri, 24 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkali wa Hip Hop Bongo, Stamina amesema, yupo tayari kurudina na aliyekuwa mkewe ambaye waliachana miaka kadhaa iliyopita.
Stamina ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na Clouds FM kuhusu masuala mbalimbali ya maisha yake ambapo alisimulia jinsi alivyoachana na mkewe baada ya kushindwana.
"Kama nilivyosema sipendi sana kutabiria yajayo lakini kama ikitokea tumekaa, tukayazungumza hakuna shinda tunaweza kuishi," alisema Stamina.
Kwenye maelezo yake mengine kwenye mahojiano hayo, Stamina alisema, aligundua umuhimu wa ndoa baada ya kutoka kwenye ndoa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live