Menu ›
Burudani
Thu, 23 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rapa wa Kenya Prezzo amesema anajutia kutumia kiasi kikubwa cha pesa kwenye harusi yake na aliyekuwa mkewe, Daisy Kiplagat mwaka 2008.
Kwenye mahojiano na POVPodcastKenya, Prezzo alisema alitumia zaidi ya TSh. Milioni 85 kwenye harusi hiyo ambayo ilikuwa ya kifahari ikihusisha mialiko ya watu mashuhuri nchini humo.
Prezzo licha ya kupata mtoto na Daisy, walitalikiana mwaka 2013. Anasema kama ingekuwa ni wakati huu, basi angefunga tu ndoa ya kawaida kwenye ofisi ya Mwanasheria na mambo yangeisha.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live