Menu ›
Burudani
Thu, 18 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Zuhura Othman Soud ‘Zuchu’ amekuja na jipya, safari hii anasema kwa Bongo, haoni msanii wa kushindana naye zaidi anaangalia wasanii wa nje.
Zuchu amefunguka hayo juzikati alipokuwa akifanya mahojiano na Wasafi TV ambapo aliweka wazi kuwa, hawezi kushindana na msanii wa ndani.
“Mimi nashindana mwenyewe na muziki wangu. Sishindani na mtu hapa Bongo maana naona kabisa natakiwa kushindana na wasanii wakubwa Afrika,” anasema Zuchu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live