First lady wa Wasafi Classic Baby, Zuhura Othuman Soud ‘Zuchu’ amesema hana tatizo na msanii mwenzake wa kike Faustina Charles ‘Nandy’ kama ambavyo maneno yameibuka mitandaoni.
Alisema, akiwa nchini Ufarasa hivi karibuni aliona maneno kuwa Nandy alimtuma Mwijaku amponde yeye lakini haikumshtua kwani alijua ni masuala ya kimuziki tu.
“Niliona ni mambo tu ya kujitafutia ugali hivyo sikujali sana. Sina tatizo na Nandy na ninampongeza kwa kufunga ndoa,” alisema Zuchu.
Zuchu alisema hata kwenye harusi ya Nandy alishindwa kwenda kwa kuwa alikuwa na kazi lakini alialikwa.
“Nampongeza kwa kweli maana kuwa mjamzito halafu ni msanii na unaolewa sio kitu rahisi. Nimemwambia hata na mimi anipe hiyo duwa aliyoomba na mimi niombe,” alisema Zuchu.