Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sina mahusiano Botion - Amber Lulu

Amberlulu Msanii wa BongoFleva Amber Lulu

Sat, 18 Sep 2021 Chanzo: Habarileo

Baada ya kusambaza video na picha akiwa ameumia usoni kwa madai ya kupigwa na mzazi mwenzake mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Lulu Euggen Amber Lulu amesema kwa sasa hayupo tena kwenye mahusiano na mwanaume huyo.

Amber Lulu ambaye anatamba na wimbo wa Nipost, amesema hawezi kumkataza mzazi mwenzake kuja kumuangalia mtoto, hivyo anapokuja hapo ni kwaajili ya kumuangalia mtoto wao Arianna.

Amesema lakini kuhusu mahusino hana mtu, hivyo watu wasimuulize maswali yoyote yupo na nani au kuhusiana na mzazi mwenzake kwakuwa tayari ameshatangaza hadi kwenye mitandao ya kijamii kwamba hayupo kwenye mahusiano.

“Stakiiii jamani sijarudiana na mtu na haitokuja kutokea ishapita huko kabisa najutaa,” amesema.

Chanzo: Habarileo