Menu ›
Burudani
Fri, 15 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aprili 3, Mwaka 1973 Mhandisi wa kampuni ya Motorola, Martin Cooper alisimama kando ya barabara ya Sixth Avenue huko mjini Manhattan nchini Marekani, mkononi akiwa ameshika kifaa chenye ukubwa wa (kitofali kidogo).
Kifaa hicho si kitu kingine, bali ilikuwa ni simu ya kwanza ya mkononi aina ya Motorola DynaTAC 8000X iliyovumbuliwa na yeye mwenyewe.
Miaka 10 baadae Septemba 21 mwaka 1983, simu hiyo ilipata kibali cha serikali cha kuingizwa sokoni rasmi kama simu ya kwanza ya mkononi.
Simu hiyo ilikuwa na uzito wa kilo moja.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live