Menu ›
Burudani
Thu, 23 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mrembo anayefanya muziki wa Bongo Fleva, Aaggy Baby ametoa kali ya mwaka baada ya kusema, hamfahamu, mrembo aliyetrend hivi karibuni Rushynah.
Kupitia mahojiano aliyoyafanya na Global TV Online, Aggy aliulizwa kabila lake na ndipo aliposema yeye ni Msukuma na alipoulizwa kuhusu kuwa na undugu na Rushynah ndipo aliposema hamjui.
"Rushynah? Ndio nani simjui labda nitamfatilia kwa kweli nilikuwa simjui," alisikika Aggy.
Licha ya Mtangazaji kumkumbusha kuwa mrembo huyo ni yule aliyekuwa mke wa Haji Manara, mrembo huyo aliendelea kushikilia msimamo wake kuwa hamjui.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live