Menu ›
Burudani
Thu, 18 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamuziki wa Nigeria Simi ‘Soft Queen’ amewatetea watoto wa kwanza kuzaliwa ‘First Born’ akisema waachwe wapumue sio kupewa zigo la majukumu na lawama.
Akifunguka hilo kupitia ujumbe alioshea mitandaoni Simi unaeleza kuwa
“Tuwaache watoto wa kwanza kuzaliwa wapumue, kuzaliwa wa kwanza haimaanishi wanaweza kubeba mzigo wa kila mtu. Wengi wao hawapendi ila hawawezi kusema”.
“Tuwaache wapumue pia watoto wa kwanza kuzaliwa wajifunze kusema Hapana na kujiwekea mipaka wanastahili amani pia”.
Vipi First Born mna lipi la kumuongezea mtetezi wenu Simi?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live