/>
Muimbaji huyo ameendelea kwa kusema hata hivyo bado muziki wake umeweza kusikika kitu ambacho anashukuru.
“Ukizungumzia moja ya wasanii ambao hawakupata bahati ya kupata nafasi kubwa kwenye radio station, mimi pia naweza kusema nipo,” amesema.
“Sikupata bahati kabisa nyimbo kupigwa kwenye radio station lakini wananchi wamenipokea, wamesema Mbosso tunakusapoti, wamenisapoti nashuru leo nimefika nilipofika,” Mbosso ameiambia Bongo5.
Utakumbuka Mbosso mwaka ndipo amejiunga na label ya WCB inayomilikiwa na Diamond Platnumz. Kuna media nne ambazo hazichezi kazi za wasanii wote waliochini ya label hiyo.