Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Siku 90 baada ya kuondolewa, Slay yarudi Netflix

48sktkqTURBXy84MDIwNTA2MDJkNmE4ZDFlZTc1Y2UwYTJkZTlkMzA5Ni5qZmlmkZUDAADNBurNA M 660x400.jpeg Mwigizaji Mtanzania, Idris Sultan

Sun, 8 Aug 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hatimaye filamu ya ‘Slay’ aliyocheza Mtanzania, Idris Sultan na wenzake kutoka nchi mbalimbali Afrika imeweza kurejea kwenye mtandao wa Netflix tangu iondolewe Mei 2, 2021.

Filamu hiyo iliwekwa Netflix Machi 26 mwaka huu, huku Idris akiweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza nchini kuingiza filamu kwenye mtandao huo mkubwa duniani kwa mauzo ya filamu.

Sababu ya kutolewa ni kutokana na kukiuka taratibu za hakimiliki ambapo filamu hiyo imetumia wimbo uitwao ‘All For You’ wa msanii, Wendy Shay kutoka Ghana bila makubaliano yoyote na mmiliki wa nyimbo hiyo.

Baada ya suala hilo kumalizika ndani ya miezi, Netflix wameirejesha filamu hiyo kwenye jukwaa lake.

Ukiachana na Idris, filamu hiyo ina wakali kama Tumi Morike, Ramsey Nouah, Fabian Adeoye Lojede, Enhle Mbali, Amanda Du-Pont, Lillian Dube na wengineo wengi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live