Unakumbuka ile shoo ya Werrason iliyoahirishwa mara mbili na kushindwa kufanyika kutokana na mvua za masika zilizonyesha jijini Dar es Salaam kwa takriban siku nne mfululizo? Sasa mkali huyo wa masauti anatua tena kutikisa Jukwaa la Life Park Mwenge kwa mara nyingine, lakini kama una tiketi ulinunua wakati ule fahamu kuwa hazitambuliki tena.
Mwandaaji wa shoo hiyo, Yale Ngos anasema hazitambui tiketi hizo na kwamba mashabiki wanaotaka kumuona Werrason wakate upya.
Mkurugenzi wa Basata, Godfrey Mngereza amesema hawajapata malalamiko kutoka kwa mashabiki na iwapo watapata taarifa hiyo rasmi watachukua hatua.
“Hatujapata taarifa hiyo sisi bado tunayatambua makubaliano ya awali kwamba mashabiki watunze tiketi sasa hili halijatufikia,” anasema Mngereza.