Menu ›
Burudani
Tue, 22 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamuziki wa nyimbo za Singeli Sholo Mwamba amesema kitu ambacho kinamuumiza kila siku kwenye maisha yake ni kutomfahamu mama yake mzazi.
Amedai kuwa mama yake alifariki wakati yeye akiwa na umri mdogo sana, hiyo basi alipofika umri wa kujitambua alionyeshwa picha ya mama yake tu.
Aidha msanii huyo anaeleza kuwa matamanio yake ni kwamba mama yake angekuwepo kwa wakati huu angefurahi sana.
Sholo hakusita kumshukuru baba yake mazazi kwa malezi aliyo mpatia akishirikiana na mama yake mlezi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live