Menu ›
Burudani
Thu, 21 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii na Mjasiriamali, Zuwena Mohamedi ( Shilole ) ametimiza umri wa miaka 36 leo December 20,2023 na ameikamilisha furaha yake kwa kujizawadia gari aina ya Toyota Prado alilojinunulia mwenyewe lenye thamani iliyotajwa kuwa ni Tsh. milioni 70 ambalo amekua akililipia taratibutaratibu kwa Kampuni iliyomuuzia.
Shilole amepigwa na mshangao baada ya kufanyiwa suprise na Wadau hao kwakuwa hawakumwambia kuwa atalipata leo gari lake licha ya yeye kutamani sana kulipata leo lakini wakamdanganya kuwa litachelewa lengo likiwa ni kumfanyia suprise katika siku yake hii muhimu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live