Msanii na mafanyabishara, Zuwena Mohamed 'Shilole' amemwambia rafiki yake, msanii wa Hip Hop Ibrahim Mussa 'Roma' arejee nchini kwani nchi ipo swari.
Shilole ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na wanahabari kwenye mgahawa wake wa Shishi Food jijini Dar alipokuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa.
"Roma rudi bwana nchi ipo swari lakini pia umeacha mke huku bwana hebu rudi. Kuna siku aliniambia anarudi mara akaniambia yupo Mbagala anazingua tu, arudi bwana," alisema Shilole.
Roma aliondoka nchini miaka kadhaa na kutimkia Marekani kwa kile kilichosemekana ni kuwa na hali mbaya ya kisiasa nchini.