Msanii na mfanyabiashara, Zuwena Mohammed 'Shilole ama Shishi Trump' amesema amemalizana kijeshi na kistaarab na Alikiba baada ya kutoleana maneno kwenye interview na mitandaoni baada ya Alikiba kusema hakumualika kwenye uzinduzi wa Album yake.
Shilole anasema kupatana ni vizuri kwa sababu maisha ni mafupi hapa duniani, pia mashabiki wategemee kuona kazi yake na Alikiba ikitoka siku sijazo.
Ikumbukwe kuwa, mwishoni mwa mwaka jana, Kiba na Shilole waliingia kwenye ugomvi mzito baada ya Alikiba kudai kuwa hakumwalika Shilole kwenye part ya uzinduzi wa albamu yake jambo ambalo lilimuibua Shilole na kutokwa na povu katika ukurasa wake wa Instagram.