Baada ya kutangaza vita na kushikilia msimamo wake wa kuondoa aina ya muziki wa Amapiano ambao umekuwa gumzo Tanzania, msanii wa Bongo Fleva Shetta ameibuka tena akiweka msisitizo kuwa yuko serious na anacho kisema.
Kupitia insta stor yake ameeandika kuwa muziki wa amapiano ambao unafanywa na wanamuziki wa Bongo haufiki popote akieleza kuwa hivi karibuni alitembelea ‘klabu’ za nchini #SouthAfrica na kusema hakuna hata ‘klabu’ moja ambayo inapigwa nyimbo za amapiano za wasanii Wakitanzania.
Akiendelea kwa kueleza kuwa miaka ya nyuma akitolea mfano wimbo wake wa ‘Kerewa’ aliyomshirikisha Diamond ulivuma sana kweye ‘televisheni’ za nje kushinda Amapiano.