Menu ›
Burudani
Tue, 5 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muigizaji Shamsa Ford amefunguka kuwa, kabla ya kuwa maarufu, amepitia msoto wa maana mpaka kufanikiwa.
Akizungumza na moja ya kituo cha radio cha jijini Dar, Shamsa amesema moja ya tukio alilopitia ni kuwahi kulala chini na mtoto wake kwa rafiki yake.
“Nishawahi kulala hadi na mwanangu...nimelala naye kabisa...tena nililala na mtoto wangu chini tena kwa rafiki yangu,” alisema Shamsa Ford.
Shamsa mbali na uigizaji, pia ni mjasiriamali. Anafanya biashara ya nguo na kwa sasa si haba, amefanikiwa!
Chanzo: www.tanzaniaweb.live