Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shakira kizimbani kwa kukwepa kulipa kodi

Shakiraaa Shakira kizimbani kwa kukwepa kulipa kodi

Wed, 28 Sep 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mahakama nchini Uhispania imeidhinisha kesi dhidi ya mwimbaji wa pop wa Colombia Shakira kuhusu tuhuma za ulaghai na kukwepa kulipa kodi.

Waendesha mashtaka wa Uhispania walimshtaki mtumbuizaji huyo mwaka wa 2018 kwa kushindwa kulipa ushuru wa euro milioni 14.5 (Sh bilioni 32.305) kwa mapato yaliyopatikana kati ya 2012 na 2014. Waendesha mashtaka wanatafuta kifungo cha miaka minane jela na faini kubwa iwapo atapatikana na hatia ya kukwepa kulipa kodi.

Shakira, 45, amekanusha mara kwa mara makosa yoyote na kukataa makubaliano na mamlaka ili kuepuka kwenda mahakamani. Kampuni yake ya mawasiliano ya umma imesema kuwa tayari amelipa kila kitu alichodaiwa na riba ya ziada ya euro milioni 3 .

Mahakama iliyoko katika mji wa Esplugues de Llobregat karibu na Barcelona ilisema kuwa Shakira atakabiliwa na makosa sita ya ulaghai wa kodi. Tarehe ya kesi bado haijatajwa.

Kesi hiyo inategemea ambapo Shakira aliishi wakati wa 2012-14. Waendesha mashtaka huko Barcelona wamedai mshindi huyo wa Grammy alitumia zaidi ya nusu ya kipindi hicho nchini Uhispania na alipaswa kulipa ushuru nchini humo, ingawa makazi yake rasmi yalikuwa Bahamas.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live