Canada imefikia uamuzi wa kupiga marufuku matumizi ya TikTok kwenye vifaa vyote vilivyotolewa na Serikali. Uamuzi huo unaanza leo.
Msemaji wa Serikali amesema kuwa uamuzi huo unafuatia tathmini iliyofanywa na Afisa Mkuu wa habari wa Canada ambao umeonyesha kiwango cha hatari na kisichokubalika kuhusu faragha na usalama.
Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeu, amesema kuna wasiwasi wa kutosha juu ya usalama unaoizunguka TikTok hivyo mabadiliko hayo yanahitajika.
Msemaji wa Kampuni ya TikTok amesema kampuni yao imesikitishwa na uamuzi huo.
Hali hii imekuja siku chache baada ya Tume ya Ulaya kutangaza marufuku kama hii kwa wafanyakazi wake.