Menu ›
Burudani
Fri, 22 Oct 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
MBUGA ya Wanyama ya Serengeti iliyopo nchini Tanzania imeshinda Tuzo ya Hifadhi Bora katika Bara zima la Afrika kwa mwaka 2021 ambapo hii inakuwa ni mara ya tatu mfululizo Hifadhi ya Serengeti inashinda Tuzo hiyo.
Serengeti ilikuwa ikichuana na Mbuga nyingne ikiwemo Kalahari Games Reserve (Botswana), Etosha (Namibia), Kidepo Valley (Uganda), Kruger (Afrika Kusini) na Masai Mara ya Kenya.
Tuzo hizo zimetangazwa na World Travel Awards (WTA) ya nchini Marekani ambapo mwaka 2019 na mwaka jana 2020 pia Serengeti ilishinda Kundi la Hifadhi zinazoongoza kwa ubora Afrika.
Chanzo: www.habarileo.co.tz