Menu ›
Burudani
Tue, 15 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakali wa masauti kutoka nchini Kenya, Sauti Sol wametamka kwa kinywa chao kwamba, Mbosso ni noma.
Kauli hiyo wameitamka wakali hao mara baada ya kutua nchini kwa ajili ya ziara ya kimuziki ambapo walipopewa mic na wanahabari wakiwa kwenye Uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere ndipo walipopiga stori kadhaa ikiwemo hiyo.
"Daah Mbosso ni noma, Mbosso yani anajua kuandika tumesikiliza hii albamu yake ni hatari," alisema mmoja wa wanamuziki hao huku mwenzake akitikisa kichwa kuashiria kwamba anaungana naye.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live