Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Saa ya Rick Ross gharama yake inanunua mji mzima

Rick Ross Saaa Saa ya Rick Ross.

Tue, 11 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ushindani unaojitokeza kati ya wasanii wa rap, nani anayeweza miliki vito vya thamani zaidi unatokea maeneo mengi na hivyo kupelekea wasanii hao kuishi kwa gharama kubwa.

Rapa kutoka nchini Marekani, Rick Ross (William Leonard Roberts II) jana alidhihirisha umiliki wake wa hivi punde wa kupindukia kwenye Instagram akionyesha saa ya mkononi ya kipekee yenye thamani ya dola milioni 20 (sawa na Tsh bilioni 4.87).

Saa, iliyoundwa na Jacob The Jeweler, ambayo ilichukua zaidi ya miaka mitatu kukamilika, ikiwa imepambwa kwa mamia ya vito vya thamani.

Wakati watu wengine mashuhuri wamewahi kuonyesha saa zao za kifahari, saa ya Ross inaweka rekodi mpya katika suala la bei na adimu, hivyo kuwazidi wengine.

Wadau wengi wametoa maoni yao kuhusu ununuzi wa saa hiyo, baadhi waonekana wakimsifu kwa umiliki wa saa hio ya gharama huku wengine wakikosoa vikali kuwa ni mbaya kwa muonekano na ni matumizi mabaya ya pesa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live