Siku ya jana Disemba 16 ni siku ambayo itakumbukwa na wapenzi wa filamu nchini Tanzania baada ya msiba mkubwa wa aliyekuwa muigiza nguli Marehemu Mohd Fungafunga maarufu kama Jengua kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.
Marehemu Mzee Jengua amefariki dunia siku ya Jumanne Disemba 15 nyumbani kwa mtoto wake Mkuranga Mkoa wa Pwani baada ya kuugua.
Mamia ya watu waliojitokeza kumuaga katika safari yake ya mwisho na kwa ajili ya kwenda kuzika kwenye makaburi ya Mburahati Jijini Dar Es Salaam.
Pia wachekeshaji na mastaa wa filamu walijitokeza kwa wingi kumshindikiza mwenzao ikiwa ni ishara ya upendo na mshikamano mkubwa walio nao baadhi ya wasanii hao ni kama Steve Nyerere, Miss Lucy Charles, Mzee Jumbo, Kingwendu, JB, Mama Kanumba, Patrick Kanumba, Bi Staa, Tito, Ringo, Tin White, Kivurande na Hashim Kambi ni baadhi ya mastaa waliojitokeza