Menu ›
Burudani
Thu, 14 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bondia wa Marekani Ryan Garcia anasema kwamba anamjua aliyemuua Tupac. Kupitia "Twitter" X ameandika;
"Mtaniamini kama nikiwaambia ninamjua aliyemuua Tupac? Wengi wenu mnajua jibu.. Ila ninaweza kuwathibitishia," amesema Ryan Garcia.
Kumbuka mwaka jana sakata la kifo cha Tupac lilichukua sura mpya baada ya mshukiwa namba moja Keef D kukiri mbele ya polisi kwamba alihusika na mauaji ya Tupac lakini alitumwa na Rapa #Diddy kwa ahadi ya dola za Kimarekani milioni 1.
Tupac aliuawa kwa kupigwa risasi huko Las Vegas, mwaka 1996.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live