Albamu mpya ya Malkia wa Mawimbi ya sauti Bongo, Hellen Majeshi maarufu Ruby ambayo ameiita Mega Experience, sasa ipo tayari.
Wakati wa utambulisho wa wimbo wake mpya KONANI, Clouds Fm, Ruby amesema, amejitahidi kupata wasanii wakali kutoka nchi mbalimbali katika albamu yake hiyo ijayo.
"Sijataka kuidondosha Tanzania yangu, watu wakae wakijua, hata wakisikia nimeenda kufanya ngoma na Beyonce na kwenye albamu ipo, msishangae mkanisikia nikiimba kiswahili mwanzo mwisho alafu kiingereza nikamwachia mwenyewe," amesema Ruby.
Kwenye wimbo wake mpya Konani, Ruby amemshirikisha G Nako Warawara na tayari unapatikana kwenye digital platforms.