Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rosa Ree ‘anyoosha maneno’ kuhusu WCB

8860 22580811 145391306075046 6994322695001210880 N TZW

Tue, 12 Jun 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Rosa Ree amejibu iwapo alishafanya mazungumzo na WCB kwa lengo la kujiunga na label hiyo.



Rosa Ree ambaye awali kabisa alikuwa katika label ya The Industry ameiambia Bongo5 kuwa hawajawahi kuzungumza hilo ila ni watu ambao wamekuwa bega kwa bega na yeye katika muziki wake.

“Hapana ilikuwa hamna, ndiyo timu mzima ya WCB wamekuwa wakinisapoti katika muziki wangu. Nafurahia hilo ila hatukuwahi kufikia hatua hiyo,”

Utakumbuka October 2017 wakati Rosa Ree anaweka wazi kumalizika kwa mkataba wake The Industry katika mahojiano na Bongo5 alijibu kuhusu hilo pia.

“Am open to anything as long as ina manufaa kwangu but hatujaongea” alisema.

Rosa Ree kwa sasa yupo katika label ya Dimo Production kutoka nchini Afrika kusini ambayo ndio imefanikisha kolabo yake ‘ Way Up’ na rapper Emtee kutoka nchini Afrika Kusini.

Loading...
Chanzo: bongo5.com