Menu ›
Burudani
Thu, 1 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
DJ maalum wa msanii Diamond Platnumz, Romy Jons amewaasa Watanzania kusali na kumuomba Mungu awape mwisho mwema.
Romy kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika; "Tusali kumuomba Mungu atujaalie mwisho mwema na atuepushe na moto wa Jahanam.
“Tunayopitia duniani ni kweli changamoto hadi inafikia kipindi mtu unakufuru!!! Tumuombe na kumshukuru Allah kwa kila jambo.
“Poleni mnaopitia changamoto katika kipindi hiki kugumu. Mlio hospitalini, mlio mtaani, mlio gerezani Allah anasikia maombi yenu msihuzunike sana ipo siku atatenda kama siyo duniani basi Akhera Insha Allah,” amesema Romy.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live