Msanii wa muziki wa Hip Hop, Roma ameulalamikia mtandao wa Instagram baada ya kufutwa video aliyo-share kwenye ukurasa wake wa Instagram akiimba wimbo wake mpya huku akiwa amevalia kanzu, raba na kofia ya Rasta kwa madai ya kuwa analeta taharuki kwa watu wa Imani fulani.
“Siku hizi Instagram, wana sharia za ajabu sana, wame delete ile video clip niliyopost juzi ya wimbo wa God colaboya Mr Shua na One6 sasa nimewatumia email kuuliza kosa nini?
“Wamenambia kosa sio wimbo ni yale mavazi kuvaa kanzu, raba na ile kofia ya rasta huku na-rap eti inaleta taharuki kiimani za watu, ni wamenionea au wako sahihi,” aliandika Roma.