Riyama Ally; ni muigizaji mkongwe wa Bongo Movies ambaye anafunguka kuwa, yeye na mumewe kipenzi, Leo Mystereo ni Mungu aliwakutanisha.
Riyama anasema Leo ambaye ni msanii wa Bongo Fleva ni ngumu kutengena naye mpaka kiyama.
Riyama anasema kuwa anamuomba sana Mwenyezi Mungu ampe maisha marefu mume wake na waishi miaka mingi na wasitengane na kama Mungu aliwaunganisha basi asitokee wa kuwatenganisha.
“Namuomba Mungu kila kukicha asije kutokea mtu yeyote akajaribu kututenganisha hata kidogo; yaani mpaka kiyama, hilo ndilo jambo la muhimu katika maisha yetu,” anasema Riyama ambaye ni mkali wa filamu za majonzi, miksa na uswazi.