Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rihanna kutumbuiza fainali za Super Bowl

Rihama Rihanna kutumbuiza fainali za Super Bowl

Mon, 26 Sep 2022 Chanzo: BBC

Mwanamuziki nyota wa Pop Rihanna ataongoza onesho la muda wa mapumziko kwenye fainali za mpira wa miguu wa Kimarekani Super Bowl itakayofanyika Februari huko Arizona, NFL imetangaza.

Mshindi huyo mara tisa wa Grammy alitangaza habari hiyo kwa kutuma picha ya mpira wenye chapa ya NFL kwenye Twitter.

Waandaaji walimwita nyota huyo mwenye umri wa miaka 34kama mtu mwenye kipaji kinachoweza kubadilisha 'vizazi’ katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Jumapili usiku.

Onesho hilo ni moja ya nafasi zinazoangaziwa zaidi katika muziki, huku tamasha la mwaka huu la dakika 14 likishuhudia watazamaji zaidi ya milioni 120, NFL ilisema.

Wanamuziki nyota walipanda kutumbuiza wakiwemo Dr Dre, Snoop Dogg, Eminem, Mary J Blige na Kendrick Lamar. Onesho hilo lilipata Tuzo la Emmy.

"Rihanna ni msanii wa kizazi kipya ambaye amekuwa na nguvu katika kipindi chote cha kazi yake," mkuu wa Muziki wa NFL Seth Dudowsky alisema.

Naye Jay-Z, ambaye kampuni yake ya burudani ya Roc Nation itasaidia kuandaa onyesho hilo, alimtaja nyota huyo kuwa "mwanamke mwenye unyenyekevu ambaye anapita kiwango cha matarajio kila kukicha".

"Mtu aliyezaliwa kwenye kisiwa kidogo cha Barbados na kuwa mmoja wa wasanii mashuhuri kabisa. Alijijenga kbiashara na burudani," aliongeza.

Chanzo: BBC