Menu ›
Burudani
Sat, 17 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Ukaribu wa Diamond na Rapper Rick Ross bado unaendelea kama kawaida.
Licha ya kutuhumiwa kufuta picha za Diamond kwenye Instagram, lakini bado Rick ameendelea kuonyesha bado wapo karibu.
Rapper huyo amemtag Diamond kwenye picha mbili ambazo ameziweka kwenye mtandao wake wa Instagram na kuibua shangwe kwa mashabiki wa muziki Bongo.
Hata hivyo inadaiwa kuwa kunauwezekano mkubwa Diamond akapata dili jipya kutoka kwa Rick Ross ambalo litatokana na bidhaa yake mpya ya dawa ya nywele na ndevu inayoitwa Rich ambayo anatarajia kuizindua April 22 ya mwaka huu.
Chanzo: bongo5.com