Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rema asitisha shoo zote hadi mwaka 2024 ili kuzingatia afya yake

Rema Artist Live Pic Rema asitisha shoo zote hadi mwaka 2024 ili kuzingatia afya yake

Thu, 30 Nov 2023 Chanzo: Radio Jambo

Rema, mwimbaji wa Nigeria, ametangaza mipango ya kughairi maonyesho yake yote ya Desemba 2023.

Katika chapisho kupitia Instagram mnamo Jumatano, mwimbaji huyo alisema hatatumbuiza kwa sababu ya wasiwasi wa kiafya.

Rema, hata hivyo, aliahidi kurudi kwenye jukwaa mwaka ujao.

"Inavunja moyo wangu kusema kwamba sitatumbuiza popote Desemba hii," alisema

"Imekuwa miaka ya kutembelea, nimepuuza afya yangu na ninahitaji muda wa kupata nafuu. 2024 tunaenda tena, nawapenda,” aliandika.

Rema, ambaye jina lake halisi ni Divine Ikubor, amekuwa akifurahia mapokezi makubwa kutoka kwa wapenzi wa muziki tangu alipoanza kujulikana.

Alisaini mkataba wa rekodi na D'Prince's Jonzing World, kampuni tanzu ya Mavin Records, mnamo 2019.

Mwimbaji huyo alitoa wimbo wake wa kwanza uliopanuliwa (EP) 'Rema' mnamo 2019.

Mwaka jana, Rema alitoa albamu yenye nyimbo 16 ‘Rave & Roses’.

Mnamo Oktoba, mwimbaji alitoa EP ya nyimbo tano inayoitwa 'Ravage'.

Mapema mwezi huu, hitmaker huyo aliwasisimua washiriki wa tamasha kwa wimbo wa 'Ravage Uprising', ndani ya ukumbi wa London wenye uwezo wa kuchukua watu 20,000 na mkusanyiko wake mzuri wa nyimbo na maonyesho ya jukwaa.

'Calm Down', wimbo wake wa hit, umeendelea kufanya nambari kwenye huduma za utiririshaji.

Huyu ni msanii wa pili wa Nigeria kutangaza kuchukua likizo ya muda kutoka kwa muziki kutokana na masuala yanayoambatana na afya.

Mwezi mmoja uliopita, Tiwa Savage alitangaza kuchukua mapumziko ya lazima baada ya kushauriwa na daktari wake kutokana na tatizo la kiafya.

Savage alisema kwamba kwa bahati mbaya, pia atalazimika kuahirisha shoo yake ya kwanza kabisa ambayo ingefanyika mjini London, Uingereza.

“Kwa wanajeshi wangu wa Savage, nimekuwa nikipambana na virusi kwa wiki za hivi karibuni na hivi leo niliamrishwa vikali kuchukua mapumziko ya sauti yangu kwa miezi kadhaa ijayo. Kwa bahati mbaya, nitalazimika kuahirisha shoo zangu zote ikiwemo shoo yangu ya kwanza ambayo ingefanyika London,” alisema kwenye taarifa.

Chanzo: Radio Jambo