Menu ›
Burudani
Wed, 15 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Miaka miwili iliyopita Staa wa muziki Burna Boy alimpandisha jukwaani Rema kwenye show yake ya 02Arena, London ambapo usiku wa kuamkia leo, Rema aliujaza ukumbi huo kwenye show yake na kufanya bonge la show.
Kabla ya Rema kupanda kwenye stage, alimshukuru Burna Boy kwa kumfungulia njia huku akisema angetamani kujumuika naye kwenye stage.
"Kabla sijapanda jukwaani, nataka kusema asante sana Burn Boy kwa kunileta jukwaani miaka 2 iliyopita. Leo ni zamu yangu ya kushinda hatua hiyo hiyo na ninatamani ungekuwa hapa kushiriki wakati huu nami. Bila kujali, ninashukuru kwa motisha."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live