Menu ›
Burudani
Tue, 16 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rayvanny au Vanny Boy; ni staa mwingine mkubwa wa muziki nchini Tanzania ambaye Jumapili ya Agosti 14, 2022 aliweka rekodi ya kufanya shoo ya kihistoria katika Tamasha la Siku ya Klabu ya Azam lililokwenda kwa jina la Azamka.
Rayvanny alishusha burudani yenye ujazo wake na kupata shangwe la mashabiki waliojazana kwenye Uwanza wa Azam Compex, Chamazi jijini Dar.
Mashabiki hao walisikika wakiimba kuwa hiyo ni salamu kwa lebo yake ya zamani ya Wasafi ambayo Rayvanny alijitoa hivi karibuni.
Mapokezi hayo ni kiashirio cha kuendelea kukubalika hata akiwa nje ya WCB.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live