Menu ›
Burudani
Fri, 3 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mke wa Msanii wa BongoFleva Barnaba "Raya" amemkalia kooni Msanii huyo huku akidai mume wake amemuoa lakini Msanii huyo bado hajiheshimu.
Kupitia Instagram kumekuwa na video clip ambayo inaonyesha ujio wa kazi ya pamoja baina ya Barnaba na Msanii wa kike kutoka kwenye Label ya Nandy Yammi wakifanya photoshoot ya project hiyo.
Mke halali wa Barnaba RayaTheBoss ameona asilifumbie macho suala hili baada ya kushare kwenye Insta Story yake maneno ambayo yanaonekana kumlenga Mume wake moja kwa moja. Raya ameandika; "Mtu umeoa lakini hujiheshimu."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live